Mkoa wa Mwanza
Mkoa wa Tanzania From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Mkoa wa Mwanza ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania. Umepakana na Geita upande wa magharibi, Shinyanga na Simiyu upande wa kusini na Mara upande wa mashariki. Ziwa la Viktoria Nyanza liko kaskazini. Ni mkoa mdogo kwa eneo lake la km2 25,233, lakini wa pili kwa idadi ya watu kwa kuwa na wakazi 3,699,872 kadiri ya sensa ya mwaka 2022 [1]. Makao makuu yako Mwanza mjini.

Mkoa una postikodi namba 33000.

Remove ads
Wilaya
Kabla ya kumegwa na kuzaa mkoa mpya wa Geita, mkoa wa Mwanza ulikuwa na wakazi 2,942,148 (sensa ya mwaka 2002) katika wilaya 8 ukiwa na eneo la 19,592 km2.
Kwa sasa wilaya ni: Ukerewe, Magu, Sengerema, Buchosa, Misungwi, Kwimba, Nyamagana na Ilemela. Jiji la Mwanza ndani yake lina wilaya za Nyamagana na Ilemela.
Remove ads
Wakazi
Makabila makubwa ya Mwanza ndio Wasukuma na Wazinza upande wa bara, halafu Wakerewe na Wakara visiwani.
Majimbo ya bunge
Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi yafuatayo:
- Buchosa : mbunge ni Dk. Charles Tizeba (CCM)
- Ilemela : mbunge ni Angelina Mabula (CCM)
- Kwimba : mbunge ni Mansoor Hirani (CCM)
- Magu : mbunge ni Kiswaga Boniventura (CCM)
- Misungwi : mbunge ni Charles Kitwanga (CCM)
- Nyamagana : mbunge ni Stanslaus Mabula (CCM)
- Sengerema : mbunge ni William Ngeleja (CCM)
- Sumve : mbunge ni Richard Mganga Ndassa (CCM)
- Ukerewe : mbunge ni Joseph Mkundi (CCM)
Tazama pia
Tanbihi
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads