Lazaro wa Bethania
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Lazaro (kwa Kiebrania אלעזר, Eleazar au Eliezer) ni mtu anayetajwa katika Injili ya Yohane: aliishi katika karne ya 1 huko Bethania, kijiji karibu na Yerusalemu, pamoja na dada zake Martha na Maria.


Yesu Kristo alifurahia urafiki wao wote, hasa alipokuwa akihiji kwenda Yerusalemu.
Katika nafasi ya mwisho ya kufanya hivyo, alimfufua siku ya nne baada ya kifo chake, jambo lililofanya wengi wamuamini kuwa ndiye Kristo, lakini pia wapinzani wake waharakishe kifo chake mwenyewe[1].
Lazaro anaheshimiwa na Kanisa Katoliki, na Waorthodoksi na wengineo kama mtakatifu.
Sikukuu yake huadhimishwa pamoja na ya dada zake[2] tarehe 29 Julai[3].
Remove ads
Michoro ya Ufufuko wa Lazaro
- Ufufuko wa Lazaro, picha takatifu ya Kirusi, karne ya 15, kazi ya Shule ya Novgorod; iko (State Russian Museum, Saint Petersburg)
- Ufufuko wa Lazaro, 1630-1631, mchoro wa Rembrandt van Rijn (Los Angeles County Museum of Art, Los Angeles)
- Ufufuko wa Lazaro (kufuatana na Rembrandt), 1890, mchoro wa Vincent van Gogh (Van Gogh Museum, Amsterdam)
- Ufufuko wa Lazaro, 1857, mchoro wa Léon Joseph Florentin Bonnat
Remove ads
Tazama pia
Tanbihi
Marejeo ya Kiswahili
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads