Nyanda za Juu za Kusini Tanzania

Mlima Wa Tanzania From Wikipedia, the free encyclopedia

Nyanda za Juu za Kusini Tanzania
Remove ads

Nyanda za Juu za Kusini ni eneo la juu katika kusini magharibi ya Tanzania, upande wa kaskazini wa Ziwa Nyasa. Nyanda za juu ni pamoja na sehemu za mikoa ya Mbeya, Njombe, Rukwa, Ruvuma, na Songwe, zikipakana na Malawi, Msumbiji na Zambia. [1] Mbeya ndio mji mkubwa katika nyanda za juu.

Thumb
Msitu wa Livingstone katika Safu ya Kipengere.

Jiografia

Nyanda za juu zinajumuisha milima, volkeno na tambarare za juu, pamoja na Milima ya Mbeya, Milima ya Poroto, Safu ya Kipengere, Mlima Rungwe, Tambarare ya juu ya Kitulo, Milima ya Umalila, na Nyanda za Juu za Umatengo. Tambarare ya Juu ya Ufipa inaenea kaskazini magharibi, kati ya Ziwa Tanganyika na Ziwa Rukwa. [2] Matawi mawili ya Bonde la Ufa la Afrika ya Mashariki yanaungana katika Nyanda za Juu za Kusini. Kwa upande wa kaskazini mashariki, pale Makambako kuna pengo linalotenganisha Nyanda za Juu za Kusini kutoka Milima ya Tao la Mashariki. [3]

Thumb
Ziwa Ngozi katika Milima ya Poroto.

Mlima Rungwe (mita 2,960 juu ya UB), na mlima Mtorwe (au: Mtove, m 2961) ndiyo vilele vya juu katika nyanda za juu. Vingine ni pamoja na Chaluhangi (m 2933) na Ishinga (m 2688) katika eneo la Kipengere, Ngozi (m 2621) katika Uporoto, na Mbeya (m 2826), Loleza (m 2656) na Pungulomo (m 2273) katika Milima ya Mbeya. [4]

Kutoka mitelemko ya kaskazini na mashariki ya Milima ya Mbeya maji hutiririka kwenye beseni la Ziwa Rukwa. Mto Ruaha Kuu ambao ni tawimto la Rufijiunapokea maji yake kutoka mitelemko za mashariki ya milima ya Mbeya na Kipengere.

Mto Songwe unapokea maji yake kutoka Milima ya Umalila ukiendelea kuwa mpaka kati ya Tanzania na Malawi. Mto Kiwira unakusanya maji kutoka mitelemko ya Milima ya Umalila, Milima ya Poroto na Mlima Rungwe.

Mto Ruhuhu unapokea maji ya sehemu ya kusini ya Safu ya Kipengere na Nyanda za Juu za Umatengo.

Mitelemko ya mashariki ya Umatengo hupeleka maji yao kwenda Mto Ruvuma.

Remove ads

Tabianchi

Usimbishaji unapatikana katika upeo kuanzia milimita 823 pale Ufipa hadi mm 2,850 kwenye mitelemko ya Mlima Rungwe.

Mvua inanyesha zaidi wakati wa Novemba hadi msimu wa mvua kwenye Aprili, ingawa maeneo ya juu hupata ukungu na mvua mwepesi hata wakati wa wa Mei hadi Agosti. Dalili ya mvua hutoka kwa mawingu ya radi ambayo yanajitokeza juu ya Ziwa Nyasa. Mitelemko inayotazama ziwa kwa ujumla hupata mvua nyingi.

Nyanda za juu ni baridi kuliko maeneo ya chini, na wastani ya joto la kila mwaka uko kati ya 13°C hadi 19°C. Miinuko juu ya mita 2000 inaweza kuona jalidi (hali chini ya °C 0) ya usiku kwenye miezi ya Juni hadi Agosti. [5]

Remove ads

Marejeo

Marejeo mengine

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads