Ardhi adimu
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Ardhi adimu (pia: metali za ardhi adimu; kwa Kiingereza: rare earth elements, rare earth metals) ni jumla ya elementi 17 za kikemia zikiwa lanthanidi 15 pamoja na Skandi na Ytri. [2] Skandi na Ytri zinahesabiwa kati ya ardhi adimu ka sababu mara nyingi hupatikana katika amana za mbale zilezile pamoja na lanthanidi, pia zina tabia za kufanana. Ardhi adimu zote ni metali.

Remove ads
Matumizi
Ardhi adimu hazikujulikana zamani hivyo hazikuwa na matumizi. Tangu kutambuliwa kuna njia nyingi za kuzitumia katika teknolojia ya kisasa, hasa vifaa elektroniki kama kompyuta, simu za mkononi, vyombo vya tiba na silaha za kisasa. Tabia zake za kupitisha umeme zimeruhusu kuunda sumaku ndogo zenye nguvu, jambo lililowezesha kuunda vifaa vidogo kama kompyuta ndani ya simu zetu.
Kutokana na upanuzi wa vifaa vya elektroniki umuhimu wa ardhi adimu huongezeka. Kwa mfano Europi inahitajika kwa kuonyesha rangi nyekundu katika skrini za runinga na kompyuta. Neodimi ni lazima kwa sumaku ndogo za kudumu katika kompyuta, injini za umeme na jenereta za rafadha.
Uthabiti wake ni muhimu katika aloi za metali zinazowezesha kutengeneza injini zenye mwendo mkubwa.
Zinatumiwa katika betri za kuchajisha upya na hivyo mahitaji yake ni makubwa kutokana na upanuzi za magari ya umeme na simu za mkononi, lakini pia jitihada za kuhifadhi umeme jua na umeme upepo.
Upatikanaji
Hata kama zinaitwa "ardhi adimu", hakuna uhaba wa elementi hizi duniani. Zilipokea jina la ardhi kwa sababu mwanzoni zilitambuliwa tu kwa umbo la oksidi ambazo kwa jumla zilitajwa pia kama "ardhi" katika miaka ya kwanza ya kemia ya kisasa. Zilitwa adimu au haba, kwa sababu ziliweza kutambuliwa mwanzoni kwa viwango vidogo tu, tena kwa matatizo. Seri, moja ya elementi hizo, ina nafasi ya 25 ukipanga elementi zote kufuatana na wingi wa akiba zake katika ganda la Dunia.
Lakini ardhi adimu hupatikana tu kwa hali ya mchanganyiko na elementi nyingine za aina hiyo, zinazofanana zote kikemia na kwa hiyo huhitaji jitihada kubwa za kuzitenganisha na kuzisafisha.
Siku hizi mzalishaji mkubwa duniani ni China iliyotoa asilimia 80 za mahitaji ya Dunia [3], ikifuatwa na Australia na 15% [4].
Serikali mbalimbali zimeona tatizo la kutegemea nchi 1 tu kwa malighafi muhimu kwa vifaa vya elektroniki, pia kulikuwa na hofu ya mahitaji kupita uzalishaji wa sasa, hivyo jitihada za kugundua akiba mbadala zilikaziwa[5].
Changamoto na hatari za kimazingira
Njia ya kawaida ni matumizi ya asidi mbalimbali zinazoacha matope ya sumu kwa viumbehai. Michakato hiyo ni ghali na kama haisimamiwi ipasavyo inaweza pia kuleta hatari kwa mazingira na afya.
Mara nyingi ardhi adimu hupatikana pamoja na elementi nururifu kama urani na thori; mchakato wa kuzichimba ardhini, kuzisafisha na kukoleza unaongeza mnururisho katika mazingira ya shughuli hizo pamoja na hatari kwa afya ya wafanyakazi na watu walio jirani[6].
Nchini Kenya akiba kubwa ya Neodimi imetambuliwa katika Kilima cha Mrima.
Orodha ya ardhi adimu
Jedwali linaorodhesha elementi 17 za ardhi adimu, namba atomia, ishara ya kikemia, asili ya majina yake, na mifano ya matumizi yake. Baadhi ya ardhi adimu zilipokea majina kutokana na wataalamu waliozigundua, na nyingine zilitajwa kwa kutegemea mahali zilipogunduliwa.
Tanbihi
Viungo vya Nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads