Visiwa vya Kanari

From Wikipedia, the free encyclopedia

Visiwa vya Kanari
Remove ads

Visiwa vya Kanari (kwa Kihispania: Islas Canarias) ni funguvisiwa la Afrika ya Kaskazini katika bahari ya Atlantiki. Viko baharini km 150 magharibi kwa Moroko. Umbali na Hispania ni masaa mawili kwa ndege.

Comunidad Autonoma de
Canarias
Jimbo la Kujitawala la Visiwa vya Kanari
Thumb
Miji MikuuSanta Cruz de Tenerife
Las Palmas de Gran Canaria
Eneo


 - jumla
 - % za Hispania



7.447 km²
1,5%

Wakazi


 - jumla (2011)
 - % za Hispania
 - Msongamano wa watu



2,117,519
4,4%
280 ab./km²

Uwakilishi bungeni


 Nafasi za bunge la wananchi (Congresso)
 Nafasi kwenye bunge la majimbo (Senato)

 

14
2

Rais wa serikali ya KanariAdán Martín Menis (CC)
Tovuti rasmiGobierno de Canarias
Thumb
Visiwa vya Kanari na Hispania

Visiwa vikubwa ni saba:

El Hierro, La Gomera, La Palma na Tenerife ambavyo vinaunda mkoa wa Santa Cruz de Tenerife,

halafu Gran Canaria, Fuerteventura na Lanzarote ambavyo vinaunda mkoa wa Las Palmas,

tena kuna visiwa vidogo sita vya Alegranza, Kisiwa cha Lobos, La Graciosa, Montaña Clara, Roque del Este na Roque del Oeste, vyote vya mkoa wa Las Palmas.

Remove ads

Utawala

Kisiasa visiwa hivyo ni kati ya maeneo ya kujitawala ndani ya ufalme wa Hispania.

Miji mikubwa ni Las Palmas de Gran Canaria (wakazi 378.628), Santa Cruz de Tenerife (wakazi 221.567), San Cristóbal de la Laguna (wakazi 141.627), Telde (wakazi 96.547) na Arona (79.377).

Miji mikuu ni Santa Cruz de Tenerife na Las Palmas de Gran Canaria. Makao ya mkuu wa serikali ya eneo huhamahama kati ya miji hiyo miwili kila baada ya miaka minne.

Remove ads

Wakazi

Jumla ya wakazi, kufuatana na sensa ya mwaka 2005 ni 1,968,280. Mkoa wa Las Palmas una wakazi 1.011.928 katika tarafa 33, mkoa wa Santa Cruz de Tenerife una watu 956.352 katika tarafa 52.

Thumb
Ramani ya Visiwa vya Kanari

Idadi ya wakazi wa visiwa vikubwa ni kama ifuatayo:

  • Tenerife - 906.854
  • Gran Canaria - 802.247
  • Lanzarote - 123.039
  • Fuerteventura - 86.642
  • La Palma - 85.252
  • La Gomera - 21.746
  • El Hierro - 10.477

Karibu wenyeji wote ni Wakristo wa Kanisa Katoliki.

Remove ads

Historia

Visiwa vya Kanari vilitembelewa zamani na wasafiri Wafinisia, Wagiriki na Waroma, baadaye na Waarabu. Katika Ulaya visiwa vilisahauliwa hadi mwaka 1400 hivi.

Visiwa vilikaliwa na wazawa walioitwa Guancha na Wahispania walipofika Kanari. Hakuna uhakika kuhusu asili yao. Wataalamu wengi hufikiri walikuwa Waberber. Wengine husema walikuwa wafungwa walioachiwa huru visiwani wakati wa Dola la Roma.

Wakati wa kufika kwa Wahispania kuanzia mwaka 1400 walikuwa na utamaduni bila chuma; wanasemekana hawakujua usafiri wa bahari.

Katika muda wa karne moja Wahispania walivamia visiwa na kukandamiza utamaduni wa wenyeji. Lugha yao imekwisha kabisa ingawa kuna bado majina ya mahali visiwani kutokana na lugha ya Kiguancha.

Baada ya Wahispania kufika Amerika, Las Palmas ilikuwa bandari muhimu ya safari za Atlantiki.

Uchumi

Kutokana na uzuri wa nchi na hali ya hewa ambayo ni poa mwaka wote utalii umekuwa nguzo ya uchumi wa visiwa vya Kanari pamoja na kilimo cha mazao ya biashara yanayopelekwa Ulaya, hasa ndizi na tumbaku.

Picha


Makala hii kuhusu maeneo ya Hispania bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Visiwa vya Kanari kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Remove ads
Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads