Zimbabwe

From Wikipedia, the free encyclopedia

Zimbabwe
Remove ads

Zimbabwe (jina rasmi: Jamhuri ya Zimbabwe) ni nchi inayopatikana Kusini mwa Afrika, bila pwani, inayopakana na Zambia kaskazini, Msumbiji mashariki, Afrika Kusini kusini, na Botswana magharibi. Ina idadi ya watu takriban milioni 16.7, ikiwa ya 73 duniani. Jiji lake kubwa zaidi na mji mkuu ni Harare. Zimbabwe imegawanyika katika majimbo 10. Inajulikana kwa historia yake ya ustaarabu wa kale, hasa mji wa mawe wa Zimbabwe Kuu, maporomoko maarufu ya Victoria Falls, na historia yake ya kisiasa, ikiwemo utawala wa muda mrefu wa Robert Mugabe na changamoto za kiuchumi zilizoshuhudiwa katika karne ya 21.

Ukweli wa haraka Jamhuri ya Zimbabwe Republic of Zimbabwe, Mji mkuu na mkubwa ...
Remove ads
Remove ads

Jina

Jina Zimbabwe linatokana na neno "dzimba dzamabwe" linalomaanisha "nyumba ya mawe" kwa lugha ya Kishona. Nyumba hiyo ya mawe, ambayo imehifadhiwa kama eneo la kihistoria, ilikuwa makao ya Ufalme wa Mutapa ambaye mfalme wake aliongoza eneo hilo miaka ya kale.

Thumb
Mikoa ya Zimbabwe.
Thumb
Pesa ya Zimbabwe hadi 2015, dollar ya Zimbabwe ilipofutwa, na Dolar ya Marekani kufanywa pesa rasmi.

Eneo

Zimbabwe imegawiwa katika mikoa 8 na miji 2 yenye hadhi ya mikoa. Imegawiwa zaidi katika wilaya 59 na kata 1,200.

Mikoa ya Zimbabwe ni:

Miji minne mikubwa ya Zimbabwe ni:

Thumb
Maporomoko ya maji (Bridal Vei), paa za mashariki
Thumb
Duka, Paa za mashariki, 1989
Remove ads

Historia

Historia ya awali

Wakazi wa kwanza huaminiwa kuwa wawindaji wa jamii ya Wasani.

Katika karne za kwanza BK walifika wahamiaji Wabantu wenye ujuzi wa kilimo na uhunzi.

Tangu karne ya 11, Zimbabwe ya leo imekuwa na falme imara kwenye njia muhimu ya biashara, hasa ufalme wa Mutapa.

Ukoloni

Kampuni ya British South Africa ya Cecil Rhodes iliweka mipaka ya sasa katika miaka ya 1890.

Koloni la Uingereza lilianzishwa mwaka 1923 kwa jina la Southern Rhodesia.

Mwaka 1965, serikali ya walowezi Wazungu ilijitangazia uhuru kwa jina la Rhodesia tu.

Baada ya miaka 14 ya kutengwa kimataifa na kupigana na raia Waafrika katika miaka ya 1970, mapatano ya mwaka 1979 yalikubali wakazi wote wawe na haki ya kupiga kura na nchi ikawa huru kweli kwa jina la Zimbabwe mwaka 1980.

Baada ya uhuru

Rais Robert Mugabe alipata umaarufu katika siasa kama mpiganaji dhidi ya ukoloni lakini pia kama aina ya dikteta aliyerudisha nyuma uchumi wa nchi.

Baada ya yeye kulazimishwa na wanajeshi kujiuzulu, tarehe 24 Novemba 2017 Emmerson Mnangagwa amekuwa rais mpya wa Zimbabwe.

Demografia

Kabila

Wakazi wengi (82%) ni wa kabila la Washona, 14% ni Wandebele, 2% ni wa makabila mengine ya Kiafrika, 1% ni machotara, Wahindi, Wazungu n.k.

Lugha

Kwa sasa lugha rasmi ni 16. Lugha kubwa ni Kishona (70%) na Kindebele (20%). Kiingereza ni lugha ya kwanza ya chini ya asilimia 2.5% za wakazi.

Dini

Upande wa dini, 84.1% ni Wakristo (hasa Waanglikana, Wakatoliki 8%, Wasabato na Wamethodisti). Waliobaki ni wafuasi wa dini asilia za Kiafrika (4.5%), ni Waislamu (0.7%), au hawana dini (10.2%) .

Remove ads

Tazama pia

Remove ads

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading content...
Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads