Qatar
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Qatar, rasmi kama Dola la Qatar (kwa Kiarabu دولة قطر) ni nchi ndogo iliyoko katika Mashariki ya Kati kwenye pwani ya kaskazini-mashariki ya Rasi ya Uarabuni ikiwa na idadi ya watu takriban milioni 3, wengi wao wakiwa wahamiaji. Qatar inapakana na Saudia upande wa kusini na inazungukwa na Ghuba ya Uajemi upande mwingine. Ina jumla ya eneo la takriban kilomita za mraba 11,571, na hivyo kuwa moja ya nchi ndogo zaidi duniani.Mji mkuu na jiji kubwa zaidi ni Doha, ambalo ni kituo kikuu cha kitamaduni na cha kiuchumi cha nchi hiyo.
Remove ads
Historia
Maeneo ya Qatar, pamoja na Falme za Kiarabu na Bahrain yalikuwa nyumbani kwa makabila madogo na chifu zao.
Tangu mwaka 1820 walikuwa na mikataba na Uingereza walipoahidi kuachana na uharamia na kupokea ulinzi wa Uingereza. Ulinzi huo ulizuia uvamizi wa Saudia katika karne ya 20.
Falme hizo zilikuwa nchi lindwa chini ya Uingereza hadi mwaka 1971, ambapo madola hayo madogo yalipata uhuru.
Remove ads
Siasa
Miaka ya mwisho Qatar imejihusisha na siasa ya Mashariki ya Kati kwa kuwapa silaha Waislamu wenye itikadi kali kama vile huko Palestina, Syria na Iraki, na hata Daish.
Kwa sababu hiyo imetengwa na nchi jirani, hasa Saudia.
Watu
Wananchi wengi wa Qatar kwa asili ni Waarabu na Waafrika (utumwa nchini ulichelewa sana kufutwa). Lakini kati ya wakazi wote, wenyeji hao ni asilimia 12 tu (313,000), yaani idadi kubwa sana si Waqatari wenyewe bali ni wafanyakazi kutoka nchi mbalimbali, hasa Uhindi (zaidi ya 21%) na nchi za kandokando yake (Nepal 16.6%, Bangladesh 12.5%, Pakistani 4.5%, Sri Lanka 4.3%), halafu Ufilipino (10%), Misri (9%) n.k.
Kiarabu ni lugha rasmi ya nchi lakini Kiingereza hutumiwa mara nyingi kwa mawasiliano ya biashara na ofisini.
Waqatari wenyewe ni Waislamu (hasa Wasuni) lakini watu kutoka nje hufuata pia dini mbalimbali: hivyo kati ya wakazi wote 65.5% ni Waislamu, 15.1% ni Wahindu, 14.2% ni Wakristo, 3.3% ni Wabuddha n.k.
Uchumi
Uchumi wote wa Qatar una msingi wa mafuta ya petroli na gesi yake. Kwa wastani wakazi wake wana kipato kikubwa kuliko watu wa nchi zote duniani.
Tazama pia
Viungo vya nje
- Qatar entry at The World Factbook (Kiingereza)
- Qatar katika Open Directory Project (Kiingereza)
- Qatar katika BBC News. (Kiingereza)
- Wikimedia Atlas of Qatar (Kiingereza)
- Key Development Forecasts for Qatar katika International Futures. (Kiingereza)
- Legal Portal Ilihifadhiwa 4 Desemba 2012 kwenye Wayback Machine. by the Ministry of Justice, including official gazette. (Kiingereza)
- Qatar Medical Care System (Kiingereza)
Nchi na maeneo ya Asia |
Afghanistan | Armenia2 | Azerbaijan | Bahrain | Bangladesh | Bhutan | Brunei | China | Falme za Kiarabu | Georgia2 | Hong Kong3 | Indonesia | Iran | Iraq | Israel | Jamhuri ya China (Taiwan) | Japani | Kamboja | Kazakhstan | Kirgizia | Korea Kaskazini | Korea Kusini | Kupro2 | Kuwait | Laos | Lebanoni | Macau3 | Malaysia | Maldivi | Mongolia | Myanmar | Nepal | Omani | Pakistan | Palestina | Qatar | Saudia | Singapuri | Sri Lanka | Syria | Tajikistan | Timor ya Mashariki | Turkmenistan | Ufilipino | Uhindi | Urusi1 | Uthai | Uturuki1 | Uzbekistan | Vietnam | Yemen | Yordani |
1. Nchi ina maeneo katika Asia na Ulaya. 2. Nchi iko Asia lakini inahesabiwa pia kati ya nchi za Ulaya kwa sababu za historia au utamaduni. 3. Eneo la pekee la China. |
![]() |
Makala hii kuhusu maeneo ya Asia bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Qatar kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
Remove ads
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads