Yakobo Mkubwa

From Wikipedia, the free encyclopedia

Remove ads

Yakobo, mwana wa Zebedayo na Salome, na kaka wa Mtume Yohane, alikuwa Myahudi wa karne ya 1 aliyepata kuwa mmoja kati ya Mitume wa Yesu walio muhimu zaidi[1].

Thumb
Carlo Crivelli, Yakobo Mkubwa, 1480 hivi, London, Victoria and Albert Museum.

Anaitwa "Mkubwa" ili kumtofautisha na Mtume mwingine mwenye jina hilohilo, Yakobo Mdogo mwana wa Alfayo.

Remove ads

Maisha ya awali

Yakobo pamoja na baba na mdogo wake walikuwa wavuvi huko Kafarnaumu kwenye Ziwa Galilaya.

Wataalamu kadhaa wanadhani walikuwa pia makuhani.

Wito wa utume

Inakadiriwa alikutana na Yesu mwaka 28.

Pamoja na mdogo wake waliitwa na Yesu Boanerghes ("wanangurumo") kutokana na umotomoto wao kitabia.

Pamoja na mitume wengine waliongozana na Yesu Kristo miaka mitatu hivi, ambapo Yakobo alionekana kuwa karibu sana na Yesu na kuchaguliwa naye kushuhudia matukio kadhaa ya pekee (ufufuo wa binti Yairo, kugeuka sura mlimani, kihoro bustanini).

Baada ya ufufuko wa Yesu

Baada ya kifo na ufufuko wa Yesu, Yakobo alishika nafasi ya maana katika jumuia ya kwanza ya Wakristo wa Yerusalemu.

Mwaka 44 hivi aliuawa na mfalme Herode Agripa I kwa upanga (Matendo ya Mitume 12:1-2), wa kwanza kumfia Yesu kati ya Mitume wake.

Heshima yake

Anaheshimiwa na Wakristo wote kama mtakatifu, hasa tarehe 25 Julai[2] huko Santiago de Compostela (Hispania, ambapo wengine wanaamini aliwahi kufika kwa umisionari).

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads