Kappa

From Wikipedia, the free encyclopedia

Kappa
Remove ads

Kappa ni herufi ya kumi katika Alfabeti ya Kigiriki. Umbo la kappa kubwa na ndogo limeendelea vilevile katika alfabeti ya Kilatini na hivyo hutumiwa vile hadi leo katika lugha zote zinazotumia mwandiko huo kama vile Kiswahili, Kiingereza na kadhalika. Matamshi yake ni "K", sawa na Kiswahili.

Ukweli wa haraka Alfabeti ya Kigiriki, Herufi za kawaida ...
Remove ads

Kwa matumizi ya tarakimu inamaanisha namba 20.

Kama neno lenye asili ya Kigiriki limepokelewa katika lugha ya Kiingereza mara nyingi herufi "C" imechukua nafasi ya "K". Sababu yake ni kwamba Waroma waliandika "k" mara nyingi kama "c" katika Kilatini maana hawakutofautisha herufi hizi mbili.

Remove ads

Matumizi ya kisayansi

Jinsi ilivyo kawaida kwa herufi mbalimbali za Kigiriki, kappa inatumiwa kama kifupisho kwa ajili ya dhana mbalimbali katika hesabu na sayansi.

Marejeo

Loading content...
Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads