Sigma

From Wikipedia, the free encyclopedia

Sigma

Sigma (Σ σ ς) ni herufi ya 18 katika Alfabeti ya Kigiriki. Inaandikwa kama σ (alama ya kawaida) au Σ (alama kubwa mwanzoni mwa majina). Kama iko mwishoni mwa neno huandikwa ς. Mfano jina Ὀδυσσεύς (Odysseus) ambamo kuna σ mbili katikati na ς mwishoni.

Ukweli wa haraka Alfabeti ya Kigiriki, Herufi za kawaida ...
Funga

Zamani za Kigiriki cha Kale ilikuwa pia tarakimu, ikiwa alama ya namba 200.

Asili ya sigma ni herufi ya Kifinisia ya shin 𐤔 .

Matamshi yake ilikuwa "s".

Katika alfabeti zinazofuata mfano wa Kigiriki ilipokelewa katika alfabeti ya Kilatini kama "S" na katika alfabeti ya Kisirili kama "С".

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.