Eta
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Eta ni herufi ya saba katika Alfabeti ya Kigiriki. Inaandikwa kama η (alama ya kawaida) au Η (alama kubwa). Zamani za Kigiriki cha Kale ilikuwa pia tarakimu, ikiwa alama ya namba 8.
Remove ads
Asili ya Eta ni herufi ya Kifinisia ya Heth (tazama makala ya H). Matamshi yake ya awali yalikuwa "h" na kwa maana hiyo alama iliingia katika alfabeti ya Kietruski na ya Kilatini. Ndani ya Kigiriki chenyewe sauti ya "h" ilipotea kwa muda na alama ilibaki kama "eta" ikimaanisha sauti ya aina ya "e".
Jinsi ilivyo kawaida kwa herufi mbalimbali za Kigiriki, eta inatumiwa kama kifupisho kwa ajili ya dhana mbalimbali katika hesabu na fizikia.
Katika fizikia eta ni alama kwa mesoni ambayo ni kipande kidogo cha atomi.
Remove ads
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads